Friday, 26 June 2015

NALILIA UZIMA LYRICS AIC SHINYANGA CHOIR

NALILIA UZIMA LYRICS AIC SHINYANGA CHOIR


Nalilia uzima, kutoka kwa Bwana

Ili nikaishi naye katika uzima,

Uzima wa milele

Shetani anaulilia uzima wangu mimi,

Anisukumia mawimbi ya kila haina

Na mateso makali X2



Anitisha ili nisimuone Bwana

Lakini nimejitoa ,  Kwa bwana kwa moyo wangu wote

Liwalo na liwe

Asukuma silaha za maangamizi, eti anisambaze,

bwana wangu kaniwekea walinzi,

Najivuna kwa bwana.  X2




Shetani hana nafasi,

kwangu mimi moyoni mwangu

yesu atawala , uzima wangu, niliopewa na bwana X2




Uzima wangu ni wa dhamani,

gharama yake kifo chake yesu,

dhamani yake ni damu yake,

bwana yesu msalabani. X2




Yesu ni nuru  moyoni mwangu,

yesu ni uzima wangu,

yesu ni ushindi , namtegemea yeye katika kila jambo,

siogopi kitu , bwana ni ngome yangu,

sibabaishwi kitu. X2




Nalilia uzima, kutoka kwa Bwana

Ili nikaishi naye katika uzima,

Uzima wa milele

Shetani anaulilia uzima wangu mimi,

Anisukumia mawimbi ya kila haina

Na mateso makali X2




yesu, u-natosha, u-natosha, wewe peke yako

shetani, u-shindwe, u-shindwe, kwa jina la yesu  X2







Anitisha ili nisimuone Bwana

Lakini nimejitoa ,  Kwa bwana kwa moyo wangu wote

Liwalo na liwe

Asukuma silaha za maangamizi, eti anisambaze,

bwana wangu kaniwekea walinzi,

Najivuna kwa bwana.  X2
















No comments:

Post a Comment